Open top menu
Wednesday, September 16, 2015

Mchezaji wa Yanga Muyu Twite akishangilia goli lake mara baada ya kuifungia Yanga goli la kwanza kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons

Mchezaji wa Yanga Muyu Twite akishangilia goli lake mara baada ya kuifungia Yanga goli la kwanza kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons
Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara timu ya Yanga imeendeleza wimbi la ushindi katika kuhakikisha inalitetea vyema taji lake baada ya leo kutoa kipigo kingine cha goli 3-0 mbele ya Tanzania Prisons ‘wajelajela’ kutoka jijini Mbeya kwenye mtanange uliomalizika jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa.

Yanga walianza kupata goli la kwanza kipindi cha kwanza kupitia kwa Mbuyu Twite aliyemalizia mpira uliomponyoka mlinda mlango wa Prisons Mohamed Yusuf na kumkuta Twite aliyeachia shuti kali akiwa hatua chache kutoka langoni.
Wakati ikiwa imeongezwa dakika moja ya nyongeza ili mchezo kwenda mapumziko, Amis Tambwe aliifungia Yanga bao la pili baada ya golikipa Mohamed Yusuf kuutema mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na kiungo wa Yanga Thabani Kamusoko na Tambwe kumalizia kwa kichwa na kuifanya Yanga kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa goli 2-0.
Mshambuliaji wa Yanga Amis Tambwe akishangilia goli lake
Mshambuliaji wa Yanga Amis Tambwe akishangilia goli lake
Kipindi cha pili kilianza kwa Tanzania Prisons kumpumzisha golikipa wao Mohamed Yusuf na kumuingiza Aron Kalambo.
Mshambuliji wa Yanga Donald Ngoma aliihakikishia Yanga ushindi mnono kwa kufunga mkwaju wa penati kufuatia James Josephat kumchezea vibaya Simon Msuva kwenye eneo la hatari. Kutokana na Josephat kumfanyia madhambi Msuva, mwamuzi aliizawadia Yanga mkwaju wa penati pamoja na kumtoa nje Josephat kwa kadi nyekundu.
Wachezaji wa Yanga wakipongezana baada ya kupata bao kwenye mchezo wao dhidi ya Tanzania Prisons
Wachezaji wa Yanga wakipongezana baada ya kupata bao kwenye mchezo wao dhidi ya Tanzania Prisons
Huo unakuwa ni ushindi wa pili mfululizo kwa klabu ya Yanga baada ya kushinda mchezo wake wa awali kwa goli 2-0 dhidi ya Coastal Union kwenye uwanja huohuo wa Taifa wakati Tanzania Prisons wao wamepoteza michezo yote miwili waliyocheza jijini Dar es Salaam. Walifungwa goli 2-1 na Azam FC kwenye uwanja wa Azam Complex kabla ya leo kuchezea kichapo cha goli 3-0 mbele ya Yanga.
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamepagawa baada ya timu yao kuvuna pointi tatu muhimu kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamepagawa baada ya timu yao kuvuna pointi tatu muhimu kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prison
Tagged
Different Themes
Written by folclassic

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

This is the most recent post.
Older Post

0 comments