Open top menu
Friday, February 15, 2013


Habari ya kushtusha iliyotokea usiku huu ni kwamba yule mshiriki wa Big Brother Africa 2012 na mwanamuziki maarufu nchini Nigeria, Goldie Harvey amefariki dunia.

Sio rahisi kuamini kwani Goldie ndo alishaianza safari ya mafanikio ya kuwa msanii mkubwa hapa Afrika na kufanya kazi na baadhi ya wasanii wakubwa ikiwemo Ambwene Yesaya kutoka Tanzania.

Taarifa inasema kuwa Goldie amefariki dunia usiku huu akiwa ndo amerudi kutoka trip yake huko Marekani, chanzo kamili cha kifo cha mwanadada huyu bado hakijawa wazi kwani tukio limetokea kwa ghafla sana usiku wa kuamkia leo.

Kwenye Facebook page na Twitter ilitumwa taarifa hii na admin wake wa account hizo, “It is with heavy heart that I have to inform you all that Goldie passed this night shortly after arriving Lagos from LA. May her soul rest in the eternal peace of the Lord – Admin!!”.

Goldie ambaye jina lake asilia ni Susan Oluwabimpe Harvey alipewa jina la "Goldie" kwasababu ya rangi asili ya nywele zake ambayo ni ya Dhahabu (Golden).
SOURCE: http://www.facebook.com/GoldieHarveyBigBrotherStarGame
Tagged
Different Themes
Written by folclassic

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments