Suma anazidi kufunguka kwa kusema kuwa kujuana na msanii huyo kulikuja wakati alipokuwa Nairobi Kenya, ambapo alitaka kufanya ngoma moja kali ndipo alipoambiwa kuwa kuna jamaa mkali yupo Nigeria anaweza kusimama vizuri, na baada ya hapo wakafanya mazungumzo na huyo jamaa, baada ya makubaliano wakamtumia beat ili aingize Chorus.
Hivyo mashabiki wake mkae mkao wa kula kupokea ujio huo mpya wa Suma Mnazaleti collabo na Mnigeria huyo baada ya kujitoa kwenye kundi la Mtanashati alipokua akifanya nao kazi awali.
0 comments