Hali
ya hatari ya zidi kupamba moto kwa wanafunzi wanao ishi maeneo ya
Kivukoni (Kigamboni ward) in Temeke
District, Dar es Salaam. Sasa hivi eneo hilo hasa nyumba na
hostel wanazoishi wanafunzi kutoka Chuo cha usimamizi wa Fedha, IFM na
wale wa Mwalimu Nyerere Memorial Academy limekuwa halitamaniki na
kutishia amani na kuwekea kikwazo shughuli za wanafunzi hao hasa katika
elimu, Matukio ya uvamizi na wizi wa laptop,simu za mikononi na pesa
yamezidi kwa kasi sana, Suala lingine ambalo limekuwa la kusikitisha ni
lile la ubakaji wa dada zetu, maana imekuwa hatari kwa wanawakewanaibiwa
na kubakwa pia,
Style
wanayoitumia watu hao ni kuvamia rooms na hostel wakiwa na mapanga huku
wamevaa mask usoni, siku si nyingi walivamia hostel iliyopo mtaa wa
Mwinyi Hamis,kigamboni na kupora simu na laptop hasa ndio lengo lao
kubwa,
Wanacholia
wanafunzi ni kutokupata support kutoka serikalini hasa jeshi la polisi
lina husika na ulinzi na usalama wa raia na mali zake, kabla sijaingia
mtamboni sasa hivi nimepata taarifa kuwa wanafunzi wa IFM wanapanga
maandamano ya amani kuelekea kwa mkuu wa polisi Dar es saalam Kamanda
Kova,
FOL
CLASSIC kupitia UNIVERSITY LENS tuna laani vikali suala hili maana
malalako haya haya jaanza kwa wanafunzi hawa, tatizo hili ni sugu vyuoni
maana hata wanafunzi wa UDSM wanaoishi Changanyikeni hukubwa na tatizo
hili mara kwa mara.
Nini kifanyike juu ya hili
toa maoni yako,kero yako na matatizo au matukio yote ya vyuoni kupitia email yetu
folclassic@gmail.com
0 comments